Magazeti leo Septemba 3,2024

DODOMA-Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ipo katika hatua za mwisho za kusaini Mkataba wa Ujenzi wa Daraja katika eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam ambapo mkataba unatarajiwa kuwa umesainiwa mwezi Septemba, 2024.









Bashungwa ameeleza hayo Septemba 2,2024 jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga aliyehoji lini Serikali itaanza rasmi ujenzi wa Daraja la Jangwani kuanzia Magomeni-Jangwani-Fire ili kuondoa hadha wanayopata wananchi wakati wa mvua.
“Serikali kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) imepanga kujenga Daraja katika eneo la Jangwani lenye urefu wa mita 390 na kimo cha mita 15 ambapo hivi sasa taratibu za manunuzi zipo katika hatua za mwisho za kusaini mkataba wake,”ameeleza Bashungwa.

Bashungwa ameeleza kuwa ujenzi wa Daraja la Jangwani utatumia fedha za mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa maendelezo ya Bonde la Mto Msimbazi.



Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news