Mashindano ya Hazina Saccoss Club yawakosha wanafunzi wa shule za sekondari nchini

NA JOSEPH MAHUMI
WF

WANANCHI wamekumbushwa kuendelea kuwaruhusu Watoto wao kujifunza Elimu ya Mikopo hasa kwa vijana wa umri wa chini na pia wao kama wazazi kuchangamkia fursa zilizopo katika vyama vya kuweka na kukopa fedha (SACCOSS) ikiwemo HAZINA SACCOSS, kwa kuwa vyama hivyo vimekuwa ni suluhisho la mikopo chechefu kwa kutoa riba nafuu ikilinganishwa na taasisi nyingine za fedha.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Tambaza wakiwasilisha kwa njia ya sanaa kuhusu huduma zinazopatikana katika Chama cha Hazina Saccoss wakati wa mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Hazina SACCOSS, Bw. Festo Mwaipaja, wakati wa Mashindano ya Hazina Club ambayo yameratibiwa na HAZINA SACCOSS na kuwakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari za Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za mkoani Dar es Salaam, ambapo wameshindania masuala mbalimbali yanayohusu masuala ya Elimu ya Fedha, Mikopo inayotolewa na HAZINA SACCOSS na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika.
Mtendaji Mkuu wa Hazina SACCOSS, Bw. Festo Mwaipaja, akizungumza jambo wakati wa mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari za Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Elimu ya Fedha, Mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Bw. Mwaipaja alisema kuwa, Mashindano hayo yamelenga kuwaanda vijana mashuleni kuwa na ufahamu wa namna ya kusimamia fedha ili kuleta tija pale ambapo wataanza kujitegemea ili wawe na nidhamu nzuri ya kusimamia fedha zao.

“Mafunzo tunayotoa hapa yatawasaidia watoto na taifa kwa ujumla kwa kuwa watawaelimisha pia wazazi wao na jamii iliowazunguka, na tutakua tumefikisha elimu kwa watanzania wengi,” amesema Bw. Mwaipaja.
Mrajisi Msaidizi Vyama vya Ushirika Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Josephat Simkoko, akizungumza jambo wakati wa mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari za Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Bw. Mwaipaja aliongeza kuwa, Changamoto ya elimu ya fedha ni kubwa duniani na endapo tukifanikiwa kupambana na changamoto hiyo ni dhahiri itafanikisha kupambana na umasikini.

Aliongeza kuwa, kwa ujumla wanafunzi waliofika katika mashindano hayo, wamepata elimu kubwa sana na itaongeza chachu ya elimu ya fedha kusambaa zaidi, mashuleni, majumbani na manufaa ya program hiyo yatakuwa makubwa katika siku za usoni.
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Minazi Mirefu, wakifuatilia moja ya wasilisho kuhusu elimu ya fedha, wakati wa mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari za Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

“Nawasihi watumishi wa umma kujiunga na HAZINA SACCOSS, kwa kuwa itawasaidia kupata mikopo ya riba ndogo sana ambayo itawasaidia hususan katika kipindi ambacho wanafunzi wanafungua shule au pale wanapopata changamoto au dharura maarufu kama “Tuliza Moyo”, na sisi tupo hapa kuwasaidia kwa kuwa ni mahali sahihi kwa watumishi,” aliongeza Bw. Mwaipaja.

Kwa upande wake Mwalimu wa Shule ya Misingi Kigogo, Bw. Florence Mafaransa, ambaye ameshiriki pamoja na Wanafunzi wake katika Mashindano hayo, alisema kuwa mashindano hayo ni muhimu kwa vijana wa taifa la kesho kwa kuwa yatawawezesha kujua namna ya kujipanga na maisha yao.
Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Mihayo Malunde, akizungumza wakati wa mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu jijini Dar es Salaam.

“Tunaishauri Serikali iendelee kutoa mafunzo kama haya kwa vijana mashuleni ili kuandaa taifa la kesho kuweza kusimamia fedha na kupata wananchi wanaokopa katika vyanzo sahihi vilivyo rasimishwa na Serikali,” amesema Bw. Mafaransa.
Shule ya Sekondari ya Tambaza wakikabidhiwa zawadi ya runinga, baada ya kuwa washindi katika sehemu ya Maswali na Majibu katika mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Elimu ya Fedha, Mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi walioshiriki mashindano hayo, Paul Mwita Sibora kutoka Shule ya Sekondari Tambaza, aliishukuru HAZINA SACCOSS kwa kuanza kutoa elimu ya fedha kuanzia ngazi ya chini kabisa kwa kuwa ni njia bora ya taifa la kesho.
Shule ya Sekondari ya Kinyerezi wakikabidhiwa zawadi ya runinga, baada ya kuwa washindi katika sehemu ya uwasilishaji wa mada katika mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.

“tutakua mabalozi bora kwa wazazi wetu na watu waliotuzunguka na kuwaeleza namna ya kujiunga na pia fursa zilizopo Hazina Saccoss,“ amesema Bw. Sibora.
Shule ya Sekondari Mzimuni wakikabidhiwa zawadi ya runinga, baada ya kuwa washindi katika sehemu ya Sanaa na Ubunifu katika mashindano ya Hazina Club yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu, Kigogo, Turiani, Mzimuni, Migombani, Minazi Mirefu, Tambaza, Makumbusho, Kambangwa na Kinyerezi, za jijini Dar es Salaam, ambapo wameshindana kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya fedha, mikopo inayotolewa na Hazina Saccoss pamoja na fursa zilizopo katika vyama vya ushirika, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kisutu, jijini Dar es Salaam.(Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam).

Mashindano hayo yanatarajiwa kuendelea nchi nzima kupitia Shule za Sekondari ikiwa na lengo kubwa la kuhakikisha vijana wa taifa la kesho wanakua na uwezo wa kusimamia vyema masuala ya fedha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news