Matumizi ya teknolojia mbadala yamepunguza gharama za ujenzi-Mhandisi Mativila

DAR-Matumizi ya Teknolojia mbadala na malighafi zinazopatikana maeneo ya kazi kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja imeweza kupunguza gharama zaidi ya asilimia 70.Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila alipotembelea banda la TARURA kwenye Maadhimisho ya 21 ya Siku ya Wahandisi katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
"Ujenzi wa madaraja na barabara kwa kutumia teknolojia ya mawe unapunguza gharama kwa asilimia 70 ukilinganisha na zege lakini pia tuna teknolojia ya kutumia kemikali kuboresha udongo unaopatikana maeneo ya kazi ili kupata ufanisi wa gharama za ujenzi,"amesema.
Ameongeza kwamba,TARURA imeweza kuondoa vikwazo sehemu zisizopitika kwa kujenga madaraja ya gharama nafuu kwa kutumia teknolojia mbadala hasa maeneo ya vijijini na kuwezesha wananchi kuzifikia huduma za kijamii na kiuchumi kwa urahisi zaidi.
"Kwa bajeti ya shilingi bilioni 1 unayoweza kujenga daraja 1 unajenga madaraja 3 ya mawe, lakini pia ukitumia udongo unaopatikana maeneo ya kazi unakuwa umepunguza gharama na mtandao mkubwa wa barabara hasa za vijijini ambapo kuna uzalishaji mkubwa wa mazao unakuwa unapitika katika Kipindi chote cha mwaka."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news