Mchango wa wachimbaji na wachakataji wadogo wa kokoto ni mkubwa-Waziri Ridhiwani Kikwete

DAR-Wajasiriamali wadogo wapatao 500 wanaojihusisha na uchimbaji na uchakataji kokoto jijini Dar es Salaam wamewezeshwa vifaa kinga na kupatiwa mafunzo ya usalama na afya ili kujiepusha na ajali, magonjwa na vifo vinavyoweza kusababishwa na vihatarishi vilivyopo katika mazingira ya kazi.
Uwezeshaji huo umefanywa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ikiwa ni utekelezaji wa jukumu lake la msingi la kujenga uelewa wa masuala ya usalama na afya miongoni mwa waajiri, wafanyakazi na wananchi kwa ujumla.
Akifungua programu hiyo ya uwezeshaji kwa wachimbaji wadogo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete amesema pamoja na changamoto zinazowakumba wachimbaji na wachakataji wadogo wa kokoto ikiwemo matumizi ya teknolojia duni na ukosefu wa mitaji, mchango wa wachimbaji hao katika uzalishaji wa malighafi za ujenzi ni mkubwa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mary Maganga amesema kwa kuzingatia mchango wa wajasiriamali wadogo katika maendeleo ya nchi, OSHA imeona ni muhimu kuwapa elimu ya usalama na afya wachimbaji hao ili waweze kuchukua tahadhari dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema mafunzo yanayotolewa na wataalam wake kwa wachimbaji wadogo yamejikita katika kuwawezesha kutambua vihatarishi vinavyoambatana na shughuli zao ikiwemo vumbi, joto kali na mtindo wa ufanyaji kazi usiozingatia taratibu za igonomia.Vifaa kinga vilivyotolewa kwa wajasiriamali hao ni pamoja na barakoa, vikinga mikono (gloves), vizibao vinavyoakisi mwanga (reflective vests) kutambulisha uwepo wa mfanyakazi mahali pa kazi pamoja na masanduku ya huduma ya kwanza.

Wajasiriamali walionufaika na uwezeshaji huo wameishukuru serikali kupitia OSHA kwa mafunzo ya usalama katika maeneo ya kazi na uwezeshaji wa vifaa kinga walivyopata.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news