Naibu Waziri Pinda akabidhi hundi ya shilingi milioni 45 kwa wajasiriamali Mpimbwe kutoka CRDB

NA MUNIR SHEMWETA
WANMM Mlele

MBUNGE wa Jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Geophrey Pinda amekabidhi hundi ya shilingi milioni 45 kwa vikundi vitatu vya wajasiriamali wa Halmashauri ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kutoka Benki ya CRDB ili kuvijengea uwezo.
Mbunge wa Jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Geophrey Pinda akikabidhi hundi ya shilingi milioni 45 kwa vikundi vitatu vya wajasiriamali wa Halmashairi ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kutoka benki ya CRDB ili kuvijengea uwezo.

Mhe Pinda amekabidhi hundi hiyo Septemba 12,2024 wakati akifungua semina ya siku moja ya kuvijengea uwezo vikundi vya wajasiriamali wanawake na vijana kunufaika na programu ya IMBEJU katika kata za halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoa wa Katavi iliyofanyika kata ya Majimoto.

Vikundi vilivyokabidhiwa kiasi hicho cha fedha ni Nguvumoja Kashishi, Imani Kashishi pamoja na kikundi kingine kitakachokidhi vigezo vya kuwezeshwa.
Sehemu ya washiriki wa semina ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wa halmashauri ya Mpimbwe iliyoendeshwa na CRDB kupitia program ya Imbeju.
Sehemu ya washiriki wa semina ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wa halmashauri ya Mpimbwe iliyoendeshwa na CRDB kupitia program ya Imbeju.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akizungumza na wajasiriamali wa Halmashairi ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati wa semina ya kuwajengea uwezo iliyoendeshwa na CRDB kupitia programu ya Imbeju. 

Akizungumza wakati wa kuzindua semina hiyo, Mhe. Pinda amesema Ili kuendesha biashara kisasa ni lazima wajasiriamali wapate ushauri na mafunzo kutoka kwa wataalamu.

Ameeleza kuwa, taasisi za fedha kama CRDB ni miongoni mwa sehemu ya uhakika ambayo mjasiriamali anaweza kupata elimu ya fedha ya uhakika ili kufanikisha mipango ya biashara.

Amewataka wajasiriamali wa Mpimbwe kutumia fursa inayolingana na uwezo wao binafsi na siyo kusikia tu benki inatoa mitaji wezeshi na kulazimika hata kudanganya ili kukopa fedha pasipo mikakati makini ya kuzitumia.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akiwa na washiriki semina ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wa halmashairi ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Ameishukuru CRDB kupitia taaasisi yake ya CRDB Foundation kwa ubunifu wa kuwafikia wajasiriamali wadogo hata waliopo pembezoni kama vile Mpimbwe.

"Hii si jambo dogo kwa taasisis inayojiendesha kibiashara kutenga bajeti ya kuelimisha wananchi na kuwapa mitaji wrzeshi," alisema Mhe. Pinda.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wajasiriamali wa vikundi alivyovikabidhi hundi ya milioni 45 wakati wa semina ya kuwajengea uwezo kata ya Majimoto halmashauri ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Washiriki wa semina hiyo ya siku moja wametoka kata za Kasansa, Mamba, Majimoto, Mwamapuli, Chamalendi, Mbede, Ikuba, Usevya pamoja na Kibaoni katika halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news