Naibu Waziri Sangu atembelea ofisi ya Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA)

DAR-Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Deus Sangu ametembelea Ofisi za Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) jijini Dar es salaam.Mhe. Sangu ametembelea ofisi hizo leo Ijumaa Septemba 13, 2024 kwa lengo la kupata taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Wakala hiyo pamoja na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali kupitia TGFA.
Katika ziara hiyo, Mhe. Naibu Waziri Sangu amepokelewa na Katibu Mkuu Ikulu, Bw. Mululi Mahendeka na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) Capt. Budodi Budodi pamoja na watumishi wengine wa wakala hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news