Ponchink City yatwaa ubingwa Kombe la Yamle Yamle, Rais Dkt.Mwinyi aahidi mema zaidi michezo Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendeleza juhudi za kuimarisha michezo kwa lengo la kuinua vipaji vya vijana.
Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Septemba 14,2024 katika Uwanja wa Gombani Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kushuhudia Fainali ya Michuano ya Yamle Yamle kati ya timu ya Ponchinki City na Wete City.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amelitaka Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC)  kuendelea kuimarisha michuano hiyo ambayo sasa imekuwa na sura ya kitaifa na kuunga mkono kila mwaka.

Katika mchezo huo wa Fainali timu ya Ponchink City imeibuka na ushindi wa bao 1-0 na kuwa mabingwa wapya wa Yamle Yamle.

Halikadhalika, Dkt.Mwinyi ameipongeza Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) kwa kuendelea kuwa wadhamini wakuu wa michuano hiyo.
Kwa upande mwingine, Rais Dkt.Mwinyi alikabidhi zawadi mbalimbali kwa wachezaji waliofanya vizuri katika michuano hiyo na kombe la Ubingwa kwa timu ya Pochinki City na shillingi milioni 20.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news