Rais Dkt.Mwinyi afungua Jukwaa la Uwekezaji la Zanzibar-Indonesia

BALI-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema,Zanzibar ina nafasi nzuri ya kujifunza mambo mbalimbali kikiwemo kilimo na usarifu wa mwani, uchimbaji mafuta na gesi, utalii, na bandari kwa Indonesia.
Ni kutokana na uzoefu, mbinu na teknolojia waliyonayo, hasa katika upande wa Uchumi wa Buluu.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Septemba 1,2024 alipofungua Jukwaa la Uwekezaji la Zanzibar-Indonesia 2024, ambalo limeandaliwa na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) katika Hoteli ya Sofitel jijini Bali, Indonesia.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amebainisha kufurahishwa na muamko wa jukwaa hilo kwa kujitokeza kwa wingi wawekezaji ambao wameonesha nia ya kuwekeza Tanzania, ikiwemo Zanzibar.

Hivyo,Watanzania watarajie wawekezaji mbalimbali, hususan katika sekta ya Uchumi wa Buluu kutoka Indonesia.
Rais Dkt. Mwinyi amewasili Bali, Indonesia tarehe 31 Agosti 2024 kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Indonesia na Afrika 2024 unaotarajiwa kuanza Septemba 2, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news