Rais Dkt.Mwinyi aishukuru Indonesian Aid kwa kuwajengea uwezo Watanzania sekta mbalimbali

BALI-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amelipongeza na kulishukuru Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Indonesia (Indonesian Aid) kwa ufadhili wa programu mbalimbali za kuwajengea uwezo Watanzania katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
Rais Dkt. Mwinyi amekutana na Bw. Tormarbulang Tobing ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Septemba 3,2024 pembezoni mwa Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Indonesia na Afrika katika hoteli ya Mulia, Bali Indonesia.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amemfahamisha Bw. Tormarbulang kuhusu dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kushirikiana na Shirika hilo katika utekelezaji wa programu mbalimbali zenye manufaa na tija kwa wananchi wa Zanzibar na kumshawishi kwa kuangalia uwezekano wa kufadhili programu za kuwajengea uwezo walengwa.

Bw. Tormarbulang Tobing amekubali ombi la Rais Dkt. Mwinyi na kumhakikishia utayari wake wa kuimarisha ushirikiano na Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news