BALI-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa anaendelea na ziara yake nchini Indonesia leo Septemba 4, 2024 ameondoka Bali kuelekea jijini Jakarta na ujumbe wake akiwemo mkewe, Mama Mariam Mwinyi.


Akiwa jijini Jakarta, Rais Dkt. Mwinyi atatembelea mashamba ya mwani, Kiwanda cha Kuchakata Mafuta ya Karafuu pamoja na Bandari.