Rais Dkt.Samia ndiye Mwenyekiti wa Jukwaa la Viongozi Wakuu wa Nchi za Afrika na China

BEIJING-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Viongozi Wakuu wa Nchi za Afrika na China mkutano unaotarajiwa kuanza Septemba 4 hadi 6,2024.
Katika ziara hiyo nchini China, Rais Dkt.Samia atashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).Atahutubia ufunguzi wa mkutano wa FOCAC.
Vilevile, Rais Samia atafanya mazungumzo na Rais China, Mhe. Xi Jinping na kushuhudia uwekaji saini wa Hati za Makubaliano ya Uboreshaji wa Reli ya TAZARA.

Katika hatua nyingine,Mheshimiwa Rais Dkt.Samia atakutana na makampuni na wawekezaji kutoka China ili kuhamasisha uwekezaji zaidi nchini Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news