Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) itaendelea kutekeleza mikakati ya kuwezesha wananchi kiuchumi-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itatekeleza mikakati mbalimbali ya kuwawezesha wananchi kiuchumi, na tayari imefanikiwa kujenga masoko katika mamlaka zote za Serikali za Mitaa Unguja na Pemba.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Septemba 20,2024 wakati wa ufunguzi wa Tamasha la Pili la Fahari ya Zanzibar, lililoandaliwa na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), katika viwanja vya maonesho ya biashara Dimani, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa,Serikali imeanzisha utaratibu mpya wa kutumia asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuweka utaratibu mzuri wa kutoa mikopo kwa makundi maalum maarufu kwa jina la 4.4.2, ikimaanisha asilimia 4 kwa wanawake, asilimia 4 kwa vijana, na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu.

Halikadhalika, Rais Mwinyi ameeleza kuwa utekelezaji wa mipango hiyo umeisaidia Serikali kuvuka malengo iliyojiwekea katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020-2025 ya kuzalisha ajira mpya laki tatu kabla ya kukamilika kwa kipindi cha miaka mitano.
Vilevile Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito kwa wajasiriamali na wafanyabiashara kujiunga na huduma zinazotolewa na ZEEA kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF).

Kwa upande mwingine, Rais Dkt. Mwinyi amewataka ZSSF kupanga mipango madhubuti itakayowahakikishia wajasiriamali wanaochangia kwenye mfuko huo kupata mafao kwa wakati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news