TAKUKURU yatunukiwa tuzo kwa kuzifanyia kazi kero za wananchi

DAR-Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) imetunukiwa tuzo na JamiiForums kwa kuwa mstari wa mbele kupokea taarifa, kero au malalamiko ya wananchi yenye viashiria vya rushwa zinazotumwa kupitia majukwaa mbalimbali ya Jamii Forums ikiwemo Fichua Uovu na kuyafanyia kazi.
Tuzo hiyo imetolewa Septemba 21,2024 jijini Dar Es Salaam katika tukio la kuwatunuku wadau wa Jamii Forums walioandika ‘Stories of Change’ zitakazoleta mabadiliko katika jamii nchini kwenye nyanja mbalimbali.
Kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu,Crispin Francis Chalamila tuzo hiyo ilipokelewa na Mkurugenzi wa Uzuiaji Rushwa wa taasisi hiyo, Bi.Sabina Seja kutoka kwa Balozi wa Umoja wa Ulaya Tanzania, Christine Grau.

Bi.Seja amesema, "Tuzo hii ina maana kubwa sana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ambayo inafanya kazi na wadau mbalimbali lwani jukumu la kuzuia vitendo vya rushwa ni la kila mwananchi.

"Jamiiforums wanapokea taarifa mbalimbali kupitia majukwaa waliyonayo, hivyo majukwaa haya yamekuwa ni fursa kwa TAKUKURU kufanya kazi kwa pamoja na wadau mbalimbali kupitia njia ya kidijitali kwenye majukwaa hayo.
"Aidha tumetunukiwa tuzo hii kwa sababu TAKUKURU tumekuwa tukichukua hatua mara moja tunapopata taarifa na wakati mwingine tumekuwa tukiwasiliana na wahusika moja kwa moja kama ikihitajika kufanya hivyo.

"Kwa hiyo majukwaa haya yanaweza kuchangia katika pande mbili, sehemu ya kwanza yanachangia katika uzuiaji pale ambapo taarifa inayotolewa inawezekana ni viashiria tu vya rushwa, lakini vitendo vya rushwa havijatendeka.
"Lakini,vile vile wakati mwingine vitendo vya rushwa vimeshatendeka, hivyo TAKUKURU inachukua hatua za kisheria kuweza kupambana na vitendo vya rushwa katika eneo hilo."

Bi.Seja amesema, majukwaa ya namna hiyo yameongeza wigo wa ushiriki wa wananchi katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news