Tanzania inaendelea kujiimarisha zaidi kidiplomasia-Waziri Mkuu

DODOMA-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kujiimarisha kidiplomasia na itaongeza nguvu zaidi ili kuwawezesha Watanzania wengi kupata fursa mbalimbali katika jumuia za kimataifa.Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikisha kuimarisha ushirikiano baina ya nchi washirika na sasa mafanikio yanaonekana.

"Rais wetu ameonesha nia njema katika kipindi chake cha miaka mitatu na nusu amefanya kazi kubwa ya kujenga diplomasia na mahusiano katika sekta mbalimbali na nchi nyingi duniani."
Ameyasema hayo leo Jumatano, Agosti 4, 2024 alipokutana na Mkurugenzi Mkuu Mteule wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika (WHO) Dkt Faustine Ndungulie, Ofisini kwake Mlimwa Jijini Dodoma.

Jitihada hizo za Serikali ya awamu ya sita zimeiwezesha Tanzania kuendelea kupaa kidiplomasia kuiwezesha nchi kupata viongozi wakubwa ndani ya Taasisi za kimataifa.

"Tunaamini kazi kubwa tulizozifanya katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya kumpata spika wa Umoja wa Mabunge duniani haikuwa kazi ndogo, na tena tumepata Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika."

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali itaendelea kumuunga mkono Mkurugenzi huyo katika utekelezaji wa majukumu yake mapya.
"Wakati wote Waziri wa Afya atakuwa karibu nawe kuhakikisha kwamba sera zetu zinaenda sambamba na malengo ya WHO, kwa uwepo wako sisi lazima tuwe msitari wa mbele kuhakikisha kwamba tunakuunga mkono kwa mipango yetu ya afya ndani ya nchi."

Kwa upande wake Mkurugenzi huyo Mtarajiwa wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika DKT. Faustine Ndungulile amemshukiru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuunga mkono na kufanya ushawishi wa kidiplomasia ili kufanikisha ushindi huo.

"Kwa upekee sana ninamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake kubwa katika kufanikisha ushindi huu kwa ushawishi wake kwenye jumuia za kimataifa pia nawashukuru viongozi wengine wa Serikali, Bunge na wadau wote."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news