PWANI-Kampuni ya TotalEnergies Marketing Ltd kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wamekabidhi madawati 130 katika shule ya Msingi Jaribuni Mpakani na Shule ya Msingi ya Kitundu za wilayani Kibiti mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ushirikiano baina yao katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kanali Kolombo ameahidi kuwa madawati hayo yatatunzwa vizuri kwa manufaa ya wanafunzi wa shule hiyo na kuongeza kuwa Wilaya ya Kibiti imekuwa ikinufaika na miradi kadhaa ya TEA ukiwemo wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Kitundu.


Bi. Ambangile ameeleza matumaini yake kwamba msaada huo utasaidia kuweka hamasa kwa wanafunzi kujifunza kwa bidii na hivyo kuchangia kukuza ufanisi na ufaulu wa shule zilizonufaika na madawati hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi wa TEA, CPA Mwanahamisi Chambega amekumbusha shule zilizonufaika na msaada huo wa madawati kuyatunza vyema.
“Miongoni mwa majukumu ya TEA ni kutafuta raslimali kutoka kwa wadau mbali mbali na kuzigawa katika taasisi za elimu ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia hivyo tunawakumbusha kutunza vifaa hivo,”amesema CPA Chambega.