Tunatekeleza mageuzi kuongeza ubora wa elimu-Waziri Mkenda

PWANI-Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema mageuzi ya Elimu yanayotekelezwa nchini yanalenga kupata wahitimu mahiri wenye ujuzi ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za ujenzi wa uchumi.
Waziri Mkenda ameeleza hayo Agosti 30, 2024 mkoani Pwani katika Mkutano wa waliokuwa Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) akimwakilisha Rais Mstaafu wa Tanzania,Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Mkenda amesisitiza kuwa, mageuzi ya Mitaala ambayo yamefanyika mpaka ngazi ya Vyuo vya ualimu yanalenga kuongeza ubora wa elimu.
"Dunia yote hii ni uwanja wa ajira kwa kila mtu, hivyo pamoja na kuwafundisha, tunapaswa kuwapatia ujuzi Vijana wetu ili waweze kujiamini na kutumia fursa mbalimbali za ajira ndani na nje ya Tanzania," amesema Prof. Mkenda.Naye Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Mkutano huo Bw. Deo Mbasa amesema Viongozi hao ambao ni Alumni wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam wamekutana kutathamini mchango wa Serikali za Wanafunzi katika kuandaa Viongozi wa kesho.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news