Uhamiaji FC yaichapa Junguni United mabao 3-1,Mafunzo yawapiga KMKM bao 1-0

NA DIRAMAKINI

UHAMIAJI FC imepiga Pira Paspoti, Pira Visa ambalo limegeuka adhabu kwa Junguni United kwa matokeo ya mabao 3-1.
Ni kupitia mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Zanzibar (PBZ Premier League) ambayo imechezwa leo Septemba 9,2024 katika Uwanja wa Annex A (Amaan Nje) jijini Zanzibar.

Licha ya Junguni United kuanza kwa bao la awali, haikuwa kikwazo kwa Uhamiaji FC kwani Abdulhafidh Salmin dakika ya 46' alisawazisha bao hilo.
Abdulbasit Said dakika ya 65' aliongeza bao la pili kwa Uhamiaji FC huku Daudi Goodluck dakika ya 85' akifunga hesabu.

Katika mchezo wa pili leo Septemba 9,2024 timu ya Mafunzo Sports Club imeibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 ni dhidi ya KMKM.

Bao la Mafunzo limefungwa na Matheo katika
Uwanja wa Annex B (New Amaan Complex) jijini Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news