Wanufaika wa Mkapa Fellow Scholarship wahitimu mafunzo ya uuguzi

MOROGORO-Wauguzi 49 wamehitimu mafunzo ya Diploma ya Uuguzi Ukunga katika Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Morogoro kupitia Mradi wa Mkapa Fellow Scholarship, unaotekelezwa na Mkapa Foundation kwa ufadhili wa Benki ya NBC.
Mafunzo haya yalitolewa ili kuboresha ujuzi na maarifa kwa wauguzi walio kwenye ajira (in-service) katika kukabiliana na changamoto za uzazi kwenye vituo vya huduma za afya wanavyofanyia kazi.

Morogoro ni miongoni mwa Mikoa inayoongoza kwa idadi kubwa ya vifo vya mama na mtoto Tanzania na kupelekea kuchagulia kwa awamu ya kwanza ya mradi huu, ambao utasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga kwa kuboresha uwezo wa kitaalamu wa wauguzi.

Mkapa Foundation imeendelea kuwa mdau muhimu katika kuboresha huduma za afya nchini kupitia eneo la rasilimali watu katika sekta ya afya. Kupitia mradi huu na kwa ufadhili wa benki ya NBC,hadi ifikapo mwaka 2028 takribani wauguzi wakunga 500 watanufaika na ufadhili huu wa masomo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news