Waziri Lukuvi atembelea banda la BoT maonesho ya Saba ya Mifumo na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi

SINGIDA-Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. William Lukuvi, ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania katika maonesho ya Saba ya Mifumo na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi yanayofanyika mkoani Singida kuanzia tarehe 06 mpaka 14 Septemba, 2024.
Katika maonesho hayo, Benki Kuu ya Tanzania inatoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake mbalimbali, ikiwemo usimamizi wa mifuko ya udhamini wa mikopo kwa niaba ya Serikali.

Mifuko hii ni pamoja na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo ya Mauzo Nje ya Nchi (Export Credit Guarantee Scheme - ECGS) na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (Small and Medium Enterprises Credit Guarantee Scheme - SME-CGS).Lengo la mifuko hii ni kuwezesha wakopaji wa sekta binafsi na wenye upungufu wadhamana na wanajihusisha na uzalishaji, kupata mitaji kutoka kwenye benki na taasisi za fedha ili kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji, mauzo ya bidhaa nje ya nchi, ajira na mapato ya taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news