Waziri Mkuu kuzindua Taarifa za Maboresho ya Mazingira ya Uwekezaji na Biashara

DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 11, 2024 atazindua Taarifa za Maboresho ya Mazingira ya Uwekezaji na Biashara pamoja na Nyenzo za Usimamizi wa Uwekezaji, katika Ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Taarifa na nyenzo hizo zitasaidia katika kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kwa kutoa mwongozo, kuboresha taratibu na kuongeza ufanisi.
Aidha, nyenzo hizo zitasaidia katika kupima maendeleo, kutatua changamoto na kuhakikisha kwamba uwekezaji unakua katika mazingira rafiki na yenye ushindani.
Viongozi wengine wanaoshiriki katika tukio hilo ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Stanslaus Nyongo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news