Balozi Mshana akutana na Waziri wa Michezo wa DRC

KINSHASA-Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mheshimiwa Said Mshana amekutana na kuzungumza na Waziri wa Michezo na Burudani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mhe. Didier Budimbu Ntubuanga.Kikao hicho kimefanyika ofisini kwa Mhe. Waziri Ntubuanga jijini Kinshasa.
Mhe. Balozi alikwenda kuonana na Mhe. Waziri kwa ajili ya kumshukuru kwa mapokezi mazuri ambayo Serikali ya DRC imeipatia timu ya Taifa ya Tanzania iliyoko nchini DRC kwa ajili ya mchezo wake na timu ya Taifa ya DRC unaotarajiwa kufanyika tarehe 10 Oktoba 2024 jijini Kinshansa nchini DRC.
Taifa Stars inakutana na Timu ya Taifa ya DRC maarufu kwa jina la Chui, kwa ajili ya mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika zinazotarajiwa kufanyika nchini Morroco mwaka 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news