Geita yapokea mradi wa shilingi bilioni 17 usambazaji wa umeme vitongoji 105

GEITA-Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martine Shigela tarehe 22 Oktoba, 2024 amempokea rasmi mkandarasi wa kampuni ya CCC (Beijing) Industrial and Commercial Ltd kutoka China.
Ikiwa ni kampuni iliyoshinda kandarasi ya Mradi wa Kusambaza Umeme kwenye vitongoji 105 vya majimbo saba (7) ya mkoa wa Geita; Mradi utakaotekelezwa katika kipindi cha miaka miwili, kuanzia sasa.

Mhe. Shigela amesema Geita imefungua ukurasa mpya wa upatikanaji wa nishati ya uhakika vijijini na kuongeza kuwa umeme utaenda kuongeza idadi ya vitongoji zaidi ya 105 na kuongeza kuwa Mradi huo, utazinufaisha pia sekta ya viwanda vidogo, madini, kilimo na uvuvi ambazo zimeajiri idadi kubwa ya watu mkoani Geita.
“Nafarijika sana kuona namna REA walivyojipanga vizuri na kuja kumtambulisha mkandarasi ili aanze kazi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji vya mkoa wetu”.

“Mkoa wa Geita una jumla ya vijiji 486 ambapo kati ya hivyo vijiji 483 vimefikiwa na huduma ya umeme kupitia Miradi ya awali inayotekelezwa na REA na kuna vitongoji 2,195, huku vitongoji 1,017 vimekwishafikiwa na huduma ya umeme, kukamilika kwa Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 105 kwenye majimbo saba (7) ya mkoa wetu, kutaongeza upatikanaji wa nishati ya umem,"amesema Mhe. Shigela.
Katika taarifa yake ya awali; Msimamizi wa Miradi ya REA mkoa wa Geita, Mhandisi, Dominick Mnaa amemwambia Mkuu wa mkoa wa Geita kuwa, Mkoa una jumla ya kata 122, vijiji 486 na vitongoji 2,195, ambapo hadi sasa jumla ya kata 121, vijiji 483 na vitongoji 1,017 vimekwishafikiwa na huduma ya umeme.

“Kata moja ya Izumacheli yenye vijiji vitatu (3) vya Izumacheli, Butwa na Lunazi bado havijafikiwa na huduma ya umeme, sababu za kutofikiwa na huduma ya umeme kwa kuwa vipo katika ziwa Viktoria hivyo basi Wakala wa Nishati Vijijin upo kwenye hatua za mwisho kutafuta mkandarasi kwa ajili ya kufikisha huduma ya umeme kwenye vijiji hivyo kwa kuwaunganishia umeme wa jua (Solar)”. Amesema, Mhandisi, Dominick.
Mhandisi, Dominick Mnaa aliyataja majimbo hayo saba (7) kuwa ni kuwa ni Geita Mjini; Geita Vijijini; Busanda; Nyang’wale; Chato; Bukombe na Jimbo la Mbogwe.

Kwa upande wa Mwakilishi wa kampuni hiyo Tanzania, Bi. Carol Wang kutoka kampuni ya CCC (Beijing) Industrial and Commercial Ltd; amesema kampuni yao imejipanga ili kukamilisha Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 105 vya mkoa wa Geita kwa haraka na ametumia fursa hiyo kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa kuahidi kuwapa usaidizi wa aina yoyote wakati wa utekelezaji wa Mradi huo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news