Magazeti leo Oktoba 17,2024

GENEVA-Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 149 wa IPU uliofanyika jijini Geneva nchini Uswisi amewataka Wajumbe wa Bunge hilo kumuamini na kumpa nafasi afanye kazi yake na waache kufikiria dhana ya Ukoloni kwa wanaofikiria hivyo ikiwemo kupinga kila kitu kwa kuwa anatokea Tanzania au Afrika. Dkt.Tulia ameyasema hayo baada ya baadhi ya wajumbe kukosoa uamuzi wake wa kufanya ziara nchini Urusi na kukutana na Rais Vladimir Putin kuhusu vita ya Ukraine badala ya kwenda Gaza ambapo,Dkt.Tulia amesema alipochaguliwa tu Novemba, mwaka jana alienda Israel na Palestine na kuonana na viongozi na kusema hajachagua upande kwenye migogoro yote na kwamba IPU inapambana kurejesha amani kwenye migogoro hiyo.
“Mimi sio Mungu, sio Malaika, ni Binadamu, nafanya kilicho ndani ya uwezo wangu, kikosi kazi kiliniambia nifanye nilichofanya kosa langu ni nini."





Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news