Magazeti leo Oktoba 6,2024

ARUSHA-Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa Cheti cha Pongezi kwa Utumishi uliotukuka katika kuwahudumia wananchi kwa Mhe. Michael Lekule Laizar ambaye alianza kuwahudumia wananchi kama Mwenyekiti wa Kijiji mwaka 1982 mpaka mwaka 1987 ambapo alichaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Mundarara na kuwatumikia wananchi kwa muda wa miaka nane.
Mwaka 1995 alichaguliwa kuwa Mbunge wa kwanza wa Longido na kuwatumikia wananchi kwa miaka 20 mpaka mwaka 2015 ambapo baadaye alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha.
Tuzo hiyo ameitoa jijini Arusha wakati wa kuhitimisha ziara yake kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Stendi ya Kilombero jijini hapo ambapo ilipokelewa na Mkuu wa Wilaya hiyo pamoja na waliowahi kuwa madiwani katika wilaya hiyo na kuhudumu na Mhe.Lekule Laizar.



Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news