Mheshimiwa Pinda akutana na Mabalozi wa SADC wanaoziwakilisha nchi zao Botswana

GABORONE-Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM),Mhe. Mizengo Pinda, amekutana na Mabalozi kutoka nchi za SADC wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana katika kikao kilichofanyika jijini Gaborone tarehe 21 Oktoba 2024.
Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Pinda amesema amewaarifu Mabalozi hao juu ya uwepo wake kama Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi ya SADC Pamoja na waangalizi wengine kutoka nchi wanachama wa SADC.
Ameeleza kuwa, amekutana nao ikiwa ni sehemu ya ratiba zake mbalimbali ili kuwasiliana nao moja kwa moja na hivyo kusaidia waangalizi kupata picha halisi ya jinsi maandalizi ya uchaguzi huo kwa ujumla yanavyokwenda.

Amesema, SEOM imejipanga na iko tayari kutekeleza jukumu lake la Uangalizi kwa ukamilifu kama walivyoaminiwa na Jumuiya na kuwatuma kuifanya kwa niaba yao.

Amesema, wao kama viongozi wa SEOM watakuwa na mikutano na watu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kusikiliza na kupata maoni ili kuhakikisha kazi yao ya uangalizi inakwenda vizuri.
Akizungumza kwa niaba ya Mabalozi hao Balozi wa Jamhuri ya Angola na Mkuu wa Mabalozi wa SADC nchini Botswana Mheshimiwa Beatriz Morais ameshukuru kukutana na uongozi wa SEOM na kuahidi kushirikiana nao ili kuhakikisha kazi yao ya uangalizi inafanyika kwa mafanikio na hivyo kuleta tija na ufanisi kwa Jumuiya na nchi inayohusika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news