Mifumo NHIF kuondoa malalamiko-Dkt.Isaka

■Ateta na Watumishi nchi nzima

■Asisitiza weledi katika kuwahudumia Wananchi

DODOMA-Maboresho makubwa ya TEHAMA yanayofanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kwenye mifumo yake ya utoaji wa huduma, yanakwenda kuondoa changamoto nyingi zilizokuwa zikisababishwa na makosa ya kibinadamu na kuwawezesha wanachama kujihudumia wenyewe bila ya kufika ofisini.Akizungumza na Watumishi wa Mfuko wa Kada ya Ofisa Udhibiti Ubora, Madai na Uanachama, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka ameweka wazi kuwa maboresho ya mifumo yanayoendelea kufanyika yanakwenda kuboresha utoaji wa huduma kwa wanachama na wadau wake wote hivyo kuongeza imani na kuridhika kwa wadau.
“Tunahitaji wadau wetu watumie mifumo zaidi katika kupata huduma hususan katika maeneo ya usajili wa wanachama na waajiri, uchakataji wa madai na usajili wa vituo vya huduma hivyo kwa upande wetu tuhakikishe tunatekeleza majukumu yetu kwa weledi mkubwa na kwa kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma,” amesisitiza Dkt. Isaka.
Amesema kuwa, matumizi ya mifumo yatarahisisha wananchi kujiunga kwa urahisi zaidi bila kuhitaji kufika katika Ofisi za Mfuko lakini pia kuondoa malalamiko yaliyokuwa yanasababishwa na ucheleweshaji wa huduma mbalimbali.
Akizungumzia mafunzo kwa maofisa hao, Dkt. Isaka amesema kuwa ni fursa nzuri kwa watumishi kujikumbusha miongozo mbalimbali, maadili ya utumishi, kubadilishana uzoefu na kupata taarifa mpya katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Baada ya mafunzo haya ambayo yamelenga maeneo ya Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, Mwongozo wa Uandikishaji Wanachama, Matekelezo na mabadiliko ya miongozo mbalimbali mtaweza sasa kuwahudumia wateja wetu vizuri na kwa wakati,” amesema Dkt. Isaka.
Amesema, katika kipindi hiki cha kuelekea utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, Mfuko umefanya maandalizi ya kutosha katika kuwahudumia wananchi wengi zaidi ili lengo la Serikali liweze kufikiwa na wanachi wawe na uhakika wa kupata huduma za matibabu wakati wowote.

...‘Bima ya Afya kwa Wote, jiunge sasa’...

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news