Rais Dkt.Mwinyi atoa pole kwa msiba wa RC mstaafu Thereza Olban Ali

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amehudhuria msiba wa aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba marehemu, Bi. Thereza Olban Ali, nyumbani kwake Miembeni, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, na marafiki leo Oktoba 15,2024.
Marehemu Bi. Thereza, wakati wa uhai wake, alikuwa mwalimu na baadaye alijiunga na Chama cha Afro Shirazi (ASP) na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Halikadhalika, aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba mwaka 1983 na alihudumu katika nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM na Jumuiya zake.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news