Rais Dkt.Mwinyi awasili Pemba kushiriki maadhimisho Siku ya Wazee Duniani

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewasili Pemba kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani.
Katika Uwanja wa Ndege wa Pemba, Rais Dkt. Mwinyi akiwa na Mama Mariam Mwinyi , walipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mattar Zahor Masoud na viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama Cha Mapinduzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama.
Dkt. Mwinyi atakuwa Mgeni Rasmi kwenye kilele cha maadhimisho ya siku wa Wazee duniani ambayo kwa Zanzibar yanaadhimishwa viwanja vya Tibirinzi, Wilaya ya Chake chake, Mkoa wa Kusini Pemba, leo tarehe 07 Oktoba, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news