ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasisitiza Mabalozi wa Nchi za Afrika wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania kuimarisha ushirikiano na fursa za kiuchumi pamoja na kuutangaza utalii wa Zanzibar kimataifa.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema wakati umefika kwa nchi za Afrika kuungana na kutumia rasilimali tulizonazo kuinua uchumi wetu na kubadilishana uzoefu ili kufikia maendeleo.
Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi amewataka mabalozi hao kuangalia fursa za ushirikiano na uwekezaji, hususan katika sekta za utalii, usafiri wa baharini na usafirishaji, uvuvi na ufugaji wa vifaranga vya samaki, mafuta na gesi, na kilimo cha viungo ambacho Zanzibar ina utajiri mkubwa.


Mabalozi hao wanatoka Burundi, Comoro, Kenya, Malawi, Misri, Morocco, Sudan, Rwanda, Uganda, na Zambia.