Rais Dkt.Samia afanya mazungumzo na ujumbe kutoka Abbott Fund

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Abbot,Bw. Robert Ford pamoja na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 3 Oktoba, 2024.
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan akiteta na ujumbe kutoka Abbott Fund ulipofika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika mazungumzo hayo.
Mwenyekiti wa Bodi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Abbot,Bw. Robert Ford akiwa katika mazungumzo hayo.

Mfuko wa Abbott ulianzishwa na Abbott mwaka 1951 kama msingi wa hisani huku ukiwekeza katika mawazo mapya yanayopanua ufikiaji wa huduma za afya, kuimarisha jumuiya mbalimbali kwa kufanya kazi na kukuza elimu ya sayansi na afya.
Aidha, mfuko huo kwa kushirikiana na wengine, hulenga kuleta matokeo ya kudumu kwa maisha ya watu na kuwatia moyo wengine kuchukua hatua chanya kwa jamii na mataifa mbalimbali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news