Rais Dkt.Samia aridhia mchakato ujenzi wa Arena kuanza Tanganyika Packers

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa ridhaa ya kuanza mchakato wa kutengeneza Arena katika viwanja vya Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam, ambapo shughuli za sanaa na burudani zitafanyika.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, alipokuwa akizungumza katika usiku wa Jukwaa la Ucheshi Wima (Cheka Tu), tukio lililopewa jina la “Kubwa Kuliko,” lililofanyika tarehe 5 Oktoba 2024 katika viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam.
Mhe. Mwinjuma amesema kuwa Serikali inaendelea na juhudi za kusaidia sekta za sanaa na michezo, pamoja na kutengeneza miundombinu muhimu kwa ajili ya shughuli hizo, ikiwemo mchakato wa ujenzi wa Arena.
“Huko tunapoelekea, hamtakuwa mnatumia nguvu nyingi kuwaleta watu kushuhudia stand-up comedy. Mhe. Rais ameshatupa ruhusa hii, na mchakato umeshaanza. Kile kilio chenu cha kupata sehemu mahsusi kwa ajili ya shughuli hii, Mhe. Rais amekisikia na ameshatupa ruhusa ya kukifanyia kazi,” alisema Mhe. Mwinjuma.
Tukio hili, ambalo ni mara ya kwanza kufanyika kwenye viwanja hivyo na kukusanya umati wa watu, pia limehudhuriwa na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete, ametoa pongezi kwa CHEKA TU kwa kutimiza miaka saba na mafanikio ambayo wameyapata mpaka sasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news