Sadaka ina Harufu:Vipi sadaka yako, yanukia inanuka?

NA LWAGA MWAMBANDE

LEO pia, msomaji wangu ninakusogezea diwani nyingine ya SADAKA INA HARUFU, ikiwa ni kitabu cha tatu kati ya vile vitano ambavyo nilivizindua Oktoba 17,2024 kupitia Moto Ulao Online Church (MUOC).
Diwani ya SADAKA INA HARUFU ni matunda ya mafundisho yanayotolewa na Mchungaji Imani Oscar Katana wa Moto Ulao Online Church (MUOC). Anatoa mafundisho kupitia mitandao ya kijamii kama WhatsApp, Facebook na YouTube.

Diwani hii imegawanyika katika sehemu tatu.

i. Mashairi yanayohusu sadaka, yenye kichwa kinachosema Toa upate kutoka na kwamba kila kitu unachokitoa ni sadaka ambayo majibu yake (Malaki 3:10-12). Moja ya beti katika sehemu hii inasema:

Sadaka ina harufu, iko mbaya iko nzuri,
Ya kuleta utukufu, hiyo usiihariri,
Na nyingine ya kukifu, Kaini ni yake mbari,
Ni vipi sadaka yako, yanukia inanuka?

ii. Mashairi yanayohusu umuhimu wa watu wanaojitoa kwako na kukuletea furaha, amani, na mafanikio, na inaitwa Kuna watu manukato.

Ukisoma na kuimba mashairi haya utapata nafasi ya kumshukuru Mungu kama unao watu kama hao pamoja na kuwaombea. Nawe utajitathmini kama ni kivuli au manukato kwa wengine na kisha utachukua hatua stahiki.

Kuna watu manukato, vizuri wananukia,
Ni miti yenye mvuto, kila mtu awania,
Kuwa nao ni kipato, maisha tafurahia,
Muumba akujalie, pata watu kama hao.

iii. Mashairi yanaeleza kwamba Mungu anafanya kitu, sisi tukifanya kitu. Tujitahidi kuwa na kitu ili Mungu afanye kitu kwetu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Ibrahimu, kwa mwanamke wa Sarepta, kwa Musa, kwa Dorkasi na wengine wengi:

Nazikumbuka talanta, zile walizogawana,
Wa tano tano kaleta, mbili mbili twaziona,
Wa moja yeye kagota, kuzalisha hakuona,
Mungu anafanya kitu, sisi tukifanya kitu.
Bofya hapa kusoma kurasa zote 34>>>

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news