ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali amesema Serikali imeweka uwekezaji mkubwa wa miundombinu ya Afya kutokana na umuhimu wa sekta hiyo kwa jamii.


Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi ameeleza juhudi za Global Fund kuisaidia Zanzibar kwenye sekta ya Afya na nyengine za maendeleo ni kuendeleza jitihada za Serikali anayoiongoza katika kutekeleza adhma ya Serikali kutoa huduma bora za afya.

Naye, Dkt. Sara Asiimwe alimueleza Rais Dk. Mwinyi kwamba Global Fund inafanya kazi kwa karibu zaidi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Sekta zake za Maendeleo ikiwemo Wizara ya Afya.
Aidha, aliiahidi Serikali kwamba taasisi yao itaendeleza ushirikiano wake na Zanzibar hasa kwenye miradi ya maendeleo.