Serikali inaendelea kuzitatua changamoto za Sekta ya Afya nchini-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema, Serikali zote mbili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinajitahidi kukabiliana na changamoto zilizomo kwenye sekta ya afya nchini.Miongoni mwa hatua amesema ni kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu, uimarishaji wa miundombinu ya afya, upatikanaji wa taarifa za afya, udhibiti wa maradhi ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza na mengineyo.
Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo Oktoba 3, 2024 wakati alipofunga kongamano la 11 la mkutano wa masuala ya Afya Tanzania, lililoshirikisha mataifa 11 duniani katika viwanja vya Maonesho ya Biashara Dimani, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha Rais Dkt. Mwinyi, amesisitiza kuwa changamoto zote zilizojadiliwa kwenye kongamano hilo, zinahitaji kuchukuliwa hatua madhubuti na za haraka, na kueleza kuwa Kongamano hilo, sio tu jukwaa la majadiliano, bali pia ni chombo cha kuchochea utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kuimarisha afya za wananchi.
Amesema, tathmini ya mkutano huo imeonesha mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta ya afya kupitia ubunifu na matumizi ya teknolojia, kama vile programu za Afya za kidigitali zinazosaidia kuimarisha huduma za afya na mifumo ya taarifa za afya.

Halikadhalika alieleza kuwa ni fursa muhimu kwa wataalamu wa afya, viongozi wa Serikali, na wadau wengine wa Maendeleo kutoka Sekta za Umma na Binafsi kuungana na kubadilishana uzoefu, kuhusu mustakabali wa Sekta ya afya Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Kongamano hilo lilikua na kauli mbiu "Kuchochea Maendeleo katika Sekta ya Afya kwa Kuunganisha Nguvu kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kwa Ajili ya Utoaji wa Huduma Bora za Afya." linahudhuriwa na washiriki 1,500 kutoka nchi 11.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news