Serikali yakutana na washirika wa maendeleo nchini

DAR-Serikali kupitia Wizara ya Fedha imebadilishana uzoefu na Washirika wa Maendeleo kuhusu ushirikiano kati ya Serikali na washirika wa maendeleo, mchakato wa bajeti ya Serikali pamoja na Mwongozo wa Usimamizi wa Miradi na Majadiliano ya Mikopo, Dhamana na Misaada katika Semina ya Ushirikiano kati ya Serikali na Washirika wa Maendeleo nchini.
Semina hiyo iliyofanyika katika Ofisi za Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) jijini Dar es Salaam imeongozwa na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Madeni kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama kwa upande wa Serikali na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), Bw. Mark Bryan Schreiner, kwa upande wa Washirika wa Maendeleo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news