DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa halmashauri nchini kuendelea kuweka mikakati ya kushirikisha sekta binafsi katika mipango ya kimaendeleo.
Amesema kuwa,kwa kufanya hivyo kutasaidia kuongeza wigo wa utoaji huduma kwa wananchi na uzalishaji wa bidhaa ikiwemo za kwenye sekta ya mifugo.



“Baraza la Madiwani kafanyeni Survey ili mzitambue vyanzo vyote na mjue vinachangia kiasi gani, nendeni mkajifunze Temeke namna walivyofanya walivyopandisha makusanyo kutoka milioni 8 kwa wiki mpaka milioni 120”.