Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha wateta na Mkurugenzi Mtendaji wa IMF

WASHINGTON D.C-Ujumbe wa Tanzania, ukiongozwa na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, umekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani (IMF), anayesimamia Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika (Africa Group 1 Constituency), Bw. Willie Nakuyanda. Katika ujumbe huo, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, alikuwepo pia.
Katika kikao hicho, Bw. Nakuyanda aliipongeza Tanzania kwa usimamizi bora wa uchumi, akisisitiza mafanikio ya programu ya "Extended Credit Facility" ambayo Tanzania inanufaika nayo kupitia IMF.
Vilevile, alielezea kuridhishwa na jinsi Benki Kuu ya Tanzania inavyotekeleza Sera ya Fedha kwa ufanisi, na kupelekea kuwa na mfumuko mdogo wa bei wa takriban asilimia 3 kwa mwaka 2024, pamoja na kuongezeka kwa upatikanaji wa fedha za kigeni nchini.
Mkutano huu ni sehemu ya mikutano ya mwaka ya IMF na Benki ya Dunia (WB) inayofanyika Washington DC, Marekani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news