Vijana wenzangu dawa za kulevya hazifai, usijiingize wala kujaribu-Frank

"Kuhusiana na dawa za kulevya, kwa uelewa wangu mimi, ninaweza nikaelezea kwa sehemu na baadhi ya sehemu kwa sababu niliwahi kutumia kwa muda wa miaka kama 10, lakini mimi nilitumia bangi.
"Ninavyoweza kuelezea, kitu cha kwanza unapotumia yanakufanya uridhike,ile hali uliyonayo uridhike nayo,mfano kipindi nikitumia bangi, mimi nilikuwa nikikosa kazi.

"Nikishavuta basi, kitu ninachosema yupo Mungu na ninajua kesho ninapata, kwa hiyo inakufanya uridhike na ukubaliane na mazingira yale.

"Bila ya kujua kwamba, pamoja na kwamba nimekosa nina hatua ninatakiwa nichukue, nifuatilie na ninaweza nikapata shughuli, kwa kweli Serikali iweke nguvu katika hili.

"Na niiombe sana, ijitahidi kuangalia mtandao huu kwa sababu wamekuwa wakishikwa watumiaji, wakishikwa na hata wanaowauzia, lakini ninajua wapo mabwana wanaowatuma na wanaowapa hao wanaowauzia hao wadogo.

"Niombe adhabu ingewekwa kubwa kwa hawa watu ambao wanatoa mizigo nje ya nchi,na kuileta ndani na kuisambaza kwa mawakala, la kuwashauri vijana wenzangu ni kwamba, madawa (dawa za) kulevya hayafai,na usijiingize wala usiseme unajaribu kwa sababu mimi kuingia ilikuwa ni kama ninajaribu.

"Kwa sababu mtaa nilioishi tulikuwa vijana wengi, na katika kutotumia kulikuwa na kauli ambayo ilikuwa inatumika kwamba usipotumia, usipofanya mambo ya kihuni, unaitwa mtoto wa mama.

"Kwa hiyo, na mimi ile sifa nikataka niikatae, ili kuwaridhisha vijana wenzangu ikabidi niingie,"Frank Charles Dida ambaye ambaye amewahi kuwa mraibu wa bangi kwa miaka 10 amebainisha;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news