Waziri Mkuu mgeni rasmi Siku ya Mwalimu Duniani wilayani Bukombe 2024

GEITA-Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Oktoba 11, 2024 amewasili mji mdogo wa Ushirombo wilayani Bukombe mkoani Geita ambapo atakuwa mgeni rasmi katika Siku ya Mwalimu Duniani kwa mwaka 2024.
Maadhimisho hayo yanafanyika kwenye Viwanja vya shule ya Sekondari Ushirombo ambapo pamoja na mambo mengine Mheshimiwa Waziri Mkuu atakabidhi vifaa vya kujifunza na kujifunzia kwa walimu na wanafunzi wilayani humo.
Mheshimiwa Majaliwa amepokelewa na Mwenyeji wake Mbunge wa Jimbo la Bukombe, ambaye ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news