HELSINK-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) amewasili nchini Finland kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 08 hadi 11 Oktoba 2024.

Katika ziara yake hiyo, Mhe. Waziri Kombo pamoja na mambo mengine, atafanya mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Elina Valtonen Oktoba 09, 2024.

Vile vile, Mhe. Kombo na ujumbe wake watashiriki mikutano ya kibbiashara inayolenga kuvutia kampuni kubwa za nchini Finland kuja kuwekeza Tanzania katika maeneo mbalimbali kama vile misitu, nishati, TEHAMA, utalii na elimu.
Katika ziara hiyo Mhe. Waziri Kombo ameambatana na viongozi waandamizi wa Serikali kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) na Mamlaka ya Kuendeleza Biashara Tanzania (TANTRADE).