ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema, Zanzibar inajikita zaidi kwenye kilimo cha viungo (Spices) kutokana na sehemu kubwa ya uchumi wake kutegemea soko la utalii ambao unachangia asilimia kubwa ya uchumi wa nchi.

Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ameleeza kuwa, eneo muhimu litakaloimarisha ushirikiano wa diplomasia baina ya Tanzania na Iran hususani katika sekta ya kilimo.
Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi alimweleza mgeni wake huyo kuhusu kuzihuisha na kuziimarisha sehemu za historia katika kukuza soko la Utalii wa Urithi na kuboresha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania hasa Zanzibar na Iran kwenye eneo hilo la utalii.
Rais Dk. Mwinyi amegusia Sekta ya Usafirishaji wa baharini na kuiomba Iran kuongeza ushirikiano kwenye eneo hilo ili kuimarisha biashara na uchumi kupitia bandari za pande mbili hizo kwa ushirikiano.


Biashara na Sekta ya Uhandisi pamoja na kuahidi kutoa ushirikiano na kubadilishana uzoefu, mbinu na teknolojia kwenye maeneo hayo.