Zanzibar ina fursa nyingi za uwekezaji-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema, Zanzibar inaendelea kuleta mageuzi makubwa ya miundombinu kwa lengo la kuwavutia wawekezaji.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Oktoba 4, 2024 Ikulu jijini Zanzibar alipokutana na Rais wa Kampuni ya Samsung C& T Corporation, Oh Se-Chul kutoka Korea Kusini na ujumbe wake.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amewahakikishia wawekezaji hao kuwa Zanzibar ina fursa nyingi na kuwakaribisha Zanzibar kuwekeza.
Halikadhalika Dkt.Mwinyi ameuelezea ujumbe huo maeneo ya vipaumbele katika uwekezaji hivi sasa kwa Zanzibar ni Utalii, Uchumi wa Buluu, Uvuvi, Usafirishaji na Mafuta na gesi.

Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza kampuni ya Samsung C&T kwa wazo la kushirikiana na nchi za Afrika hasa za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika nyanja mbalimbali za uwekezaji pamoja na kuanzisha ofisi yao Tanzania. Naye, Rais wa Kampuni hiyo, Bw. Oh Se-Chul amemuelezea Rais Dkt. Mwinyi kwamba, Kampuni hiyo katika kutanua wigo wa uwekezaji, kwa sasa imeamua kuja Afrika na Tanzania kuwa kipaumbele kwenye uwekezaji wao pamoja na kufungua ofisi zao hapa nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news