
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari (kushoto) leo Oktoba 07, 2024 ametembelea vituo vya kuandikishia Wapiga Kura katika Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar katuika siku ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Visiwani Zanzibar. Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Zanzibar umeanza leo Oktoba 07 hadi Oktoba 13, 2024 na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Wananchi wakiwa katika moja ya vituo vya kujiandikisha kuwa Mpiga Kura katika Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi wakisubiri kuandikishwa na kuboresha taarifa zao. Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Zanzibar umeanza leo Oktoba 07 hadi Oktoba 13, 2024 na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari (kushoto) leo Oktoba 07, 2024 ametembelea vituo vya kuandikishia Wapiga Kura katika Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar katuika siku ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Visiwani Zanzibar. Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Zanzibar umeanza leo Oktoba 07 hadi Oktoba 13, 2024 na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari akizungumza jambo na wananchi waliojitokeza katika Kituo cha Skuli ya Sekondari ya Mfenesini Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar kwaajili ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Zanzibar umeanza leo Oktoba 07 hadi Oktoba 13, 2024 na vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Wananchi waliojitokeza katika vituo vilivyopo Jimbo la Mtoni katika kituo cha SUZA Beilt Eil Ras ambacho kinahudumia wananchi wa Shehia ya Kibweni, Wilaya ya Mgaharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari akiangalia mwananchi aliyefika kujiandikisha akiweka saini katika kishkwambi katika moja ya vituo vilivyopo SUZA Beilt Eil Ras.
Moja ya mawakala kutoka vyama mbalimbali vya siasa waliopo katika vituo vya kuandikishia Wapiga Kura.


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Balozi Omar Ramadhan Mapuri akitoka katika moja ya vituo baada ya kukitembelea leo Oktoba 07, 2024 vituo vya Kuandikisha Wapiga Kura Mkoa wa Kusini Pemba na Kaskazini Pemba.
Wananchi mbalimbali wakiwa vituoni kuandikishwa na kuboresha taarifa zao.
Mwananchi akichukuliwa picha.

Uboreshaji wa Daftari Zanzibar unaendelea hadi tarehe 13 Oktoba, 2024 na vituo vinafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

Wananchi wakivuta subra kuelekea kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.