NA GODFREY NNKO
SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL) limeanza rasmi kutoa huduma zake tena kutoka Dar es Salaam hadi Johannesburg nchini Afrika Kusini.
Hatua hiyo ya kihistoria imeanza tena leo asubuhi ya Novemba 30,2024 kwa kutumia ndege mpya ya B737-9 Max kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).
Walioshuhudia hafla hiyo ni Mhe. Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Uchukuzi, Mhe. James Bwana, Balozi wa Tanzania, Afrika Kusini, Mhe. Balozi John Ulanga kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

ATCL ilisitisha rasmi safari zake kati ya Dar es Salaam na Johanessburg nchini Afrika Kusini, kuanzia Oktoba 7, 2019 ambapo abiria ambao walikuwa wamekata tiketi wakati huo kwa ajili ya usafiri huo walirudishiwa nauli zao.

ATCL ambayo ilikuwa ikifanya safari hiyo mara nne kwa wiki kwa maana ya Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili iliacha kufanya safari kati ya miji hiyo Agosti 23,2019 baada ya ndege yake aina ya Airbus A220-300 kuzuiliwa katika Uwanja wa Oliver Tambo jijini Johannesburg kwa amri ya Mahakama Kuu ya Guateng.

Falsafa ya 4R za Rais Dkt.Samia inajikita katika masuala ya Maridhiano (Reconciliation), Ustahamilivu (Resilience), Mageuzi (Reforms) na Kujenga upya Taifa (Rebuilding).