RUKWA-Naibu Waziri, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ma Utawala Bora Mhe.Deus Sangu amesisitiza umuhimu wa Wananchi wa Jimbo la Kwela kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa huku akibainisha kuwa uchaguzi huu ni fursa kwa wananchi kupata viongozi wa karibu wanaojua changamoto zinazowakabili za moja kwa moja katika maeneo yao.


Amesisitiza kuwa ushiriki wa kila raia ni muhimu katika kuhakikisha mchakato wa uchaguzi unafanikiwa kwa haki na uwazi, huku akiwapongeza wale ambao tayari wamepiga kura kwa kuwa mfano mzuri wa uzalendo.