SHANGHAI-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameendelea na ziara yake jijini Shanghai, China leo na kukutana na ujumbe ulioongozwa na Bw. Bai Yin Zhan kutoka kampuni ya China Harbour Engineering Co. Ltd, waliofika katika jengo la Ling Hang Group.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo katika mchakato wa kuipa dhamana kampuni hiyo ya China Harbour Engineering Co. Ltd kujenga Bandari ya Mangapwani, Unguja.

Wakati huo huo, Rais Dkt.Mwinyi amekutana na wawakilishi wa kampuni mbalimbali ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza Zanzibar, zikiwemo Fuhai Group, inayojihusisha na masuala ya nishati, mafuta, na gesi; Chery Holding Group Co. Ltd, iliyobobea katika utengenezaji wa magari yanayotumia nishati ya umeme; na China Sinopharm International, kampuni kubwa inayotengeneza madawa ya binadamu.

📅 06 Novemba 2024
📍Shanghai, China