DAR-Timu ya maafisa kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika (Tanzania Cooperative Development Commission-TCDC) ikiongozwa na Mratibu wa mradi wa uhamasishaji na uanzishaji wa Vyama vya Ushirika Mrajis Msaidizi Ibrahim Kadudu imekutana na kufanya majadiliano na Mashirika ya Agriterra pamoja na USAID Farmer to Farmer Programme.

Masuala mbalimbali yamejadiliwa yakiwemo upatikanaji wa masoko, mitaji, pembejeo, miundo mbinu ya umwagiliajipamoja na utunzaji wa mazao.

Aidha, Kadudu ameeleza kuwa kazi hiyo ya kukutana 9na wadau inatekelezwa kwa Mikoa ya Iringa, Arusha na Dar Es Salaam ikiwa ni hatua ya awali na kuendelea kwa Mikoa mingine yenye wadau wengi wa mazao ya mbogamboga na bustani.
Tags
Habari
Kilimo Tanzania
Tanzania Cooperative Development Commission (TCDC)
TCDC Tanzania
Tume ya Maendeleo ya Ushirika