ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi leo Novemba 15,2024 amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika ibada ya sala ya Ijumaa Msikiti wa Maungani Wilaya ya Magharibi B.


Wakati huo huo, Alhaj Dkt. Mwinyi baada ya sala ya Ijumaa aliendeleza utaratibu wake wa kuwatembelea Wananchi na kuwajulia hali Wagonjwa katika maeneo mbalimbali.

Msanii Mkongwe wa sanaa za Filamu na Maigizo Zanzibar Bibi Mwanamwema Khamis Juma, maarufu Bi Njiwa.
Mwingine ni Bi. Halima Muhamed, Mjane wa aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama, Marehemu Borafya Silima wanaoishi Mwera Mtofaani.