DAR-Naibu wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Hamis Mwinjuma, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Chama cha Kriketi Tanzania, Dkt. B.S. Sree Kumar, ambapo wamejadili kuendeleza mchezo huo shuleni.

Dkt. Kumar amewasilisha ombi kwa Mhe. Naibu Waziri Mwinjuma kuwa, mchezo wa Kriketi uwe miongoni mwa michezo itakayochezwa kwenye mashindano ya UMISSETA mwaka 2025.
Mhe. Naibu Waziri ameahidi kulifanyia kazi ombi hilo na Wizara itafanya mawasiliano na Ofisi ya Rais TAMISEMI ili kuona uwezekano wa mchezo huo kuongezwa kwenye michezo ya UMISSETA.