ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemuapisha Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Hamid Seif Said hafla iliyofanyika Ikulu, Zanzibar.

Ameyataja maeneo yake ya kipaumbele katika utendaji wake ni pamoja na usafi wa mji, elimu, afya, utalii wenye tija na huduma bora pamoja na kuimarisha usalama na utendaji wa kidijitali utakaoleta ufanisi.
Kabla ya uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Mjini, ndugu Hamid alikuwa Mkuu wa Wilaya ya kaskazini B.'